Kama tungeliingia ndani ya Mahali Patakatifu, ambapo ni Nyumba ya Mungu, kitu cha kwanza ambacho tungelikiona ni kinara cha taa, meza ya mikate ya wonyesho, na madhabahu ya uvumba. Madhabahu ya uvumba iliwekwa mbele ya lango la kuingia Patakatifu pa Patakatifu, mahali ambapo kiti cha rehema kilikuwa kimewekwa, yaani baada ya kukipita kinara cha taa na meza ya mikate ya wonyesho. Urefu na upana wa madhabahu hii ya uvumba ulikuwa ni dhiraa moja, wakati kimo chake kilikuwa ni dhiraa mbili. Katika Biblia, dhiraa ni takribani sentimita 45-50 kwa vipimo vya hivi sasa. Hivyo, madhabahu ya uvumba ilikuwa na mraba mdogo wenye vipimo vya takribani sentimita 50 kwa urefu na upana na sentimita 100 kwa kimo. Kama ilivyokuwa kwa madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, madhabahu ya uvumba pia ilikuwa na pembe katika zake nne za juu. Hali ikiwa imetengenezwa kwa mti wa mshita, madhabahu ya uvumba ilikuwa imefunikwa yote kwa dhahabu.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Ndani ya Hema Takatifu la Kukutania kulikuwa kumegawanyika katika sehemu kuu mbili: Mahali Patakatifu na Patakatifu pa Patakatifu. Kulikuwa na pazia kati ya sehemu...
Kifungu hiki kinaelezea juu ya nguzo, lango la pazia, mapazia ya kitani safi ya kusokotwa, mikanda, vishikizio, vikuku vya shaba, na vigingi vya shaba...
Hebu sasa tukiangalie kifuko cha kifuani ambacho Kuhani Mkuu alikitumia katika kuwahukumu watu wa Israeli. Kifungu cha maandiko hapo juu kinatueleza kuwa kifuko cha...