Kifungu hiki kinaelezea juu ya kinara cha taa cha Hema Takatifu la Kukutania. Leo nitapenda kuelezea juu ya maana ya kiroho ya vikombe hivi vya mapambo, maua na taa. Mungu alimwamuru Musa kutengeneza kwamba mhimili wa taa ili kutengeneza kinara cha taa cha dhahabu. Hivyo, kitu cha kwanza kilichofanyika ilikuwa ni kutengeneza huo mhimili, kisha baada ya huo mhimili yaliunganishwa matawi pembeni yake. Kila upande wa huo mhimili kulitengenezwa matawi matatu, kisha katika kila tawi kulikuwa na mabakuli matatu mfano wa ua la lozi, kisha vikombe vya mapambo na maua vilitengenezwa. Vivyo hivyo, taa saba ziliwekwa juu ya matawi hayo ili kuuangaza. Hivyo kinara cha taa kiliweza kuangaza vizuri kabisa ndani ya Patakatifu pa Patakatifu pamoja na vyombo vyake vya ndani.
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Mbao zote za Hema Takatifu la Kukutania mahali ambapo Mungu alikaa zilikuwa zimefunikwa kwa dhahabu. Mungu alimwambia Musa kutengeneza vikuku vya fedha ili kuushikiza...
Kama tungeliingia ndani ya Mahali Patakatifu, ambapo ni Nyumba ya Mungu, kitu cha kwanza ambacho tungelikiona ni kinara cha taa, meza ya mikate ya...
Kifungu hiki kinaelezea juu ya nguzo, lango la pazia, mapazia ya kitani safi ya kusokotwa, mikanda, vishikizio, vikuku vya shaba, na vigingi vya shaba...