Hebu sasa tukiangalie kifuko cha kifuani ambacho Kuhani Mkuu alikitumia katika kuwahukumu watu wa Israeli. Kifungu cha maandiko hapo juu kinatueleza kuwa kifuko cha kifuani cha hukumu kilitengenezwa kwa kitambaa kilichokuwa na mraba unaolingana kwa vipimo kwa urefu na upana wake. Kitambaa hiki kilikuwa kimefumwa kiujuzi kwa nyuzi za dhahabu, za bluu, za zambarau, na nyekundu na kitani safi ya kusokotwa. Vito kumi na mbili vya thamani viliwekwa katika kitambaa hiki huku kila mstari ukiwa na vito vitatu na hivyo kufanya jumla ya mistari minne. Pia Mungu alimwambia Musa kuweka Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu. Urimu na Thumimu zina maanisha ni ‘mwanga na ukamilifu.’
https://www.bjnewlife.org/
https://youtube.com/@TheNewLifeMission
https://www.facebook.com/shin.john.35
Leo hii hebu tuangalie katika kumsimika Kuhani Mkuu. Hapa tunaona kwamba Mungu alimwamuru Musa jinsi yay kumsimika Haruni na wanawe kwa kina. Neno “kusimika”...
Leo tutakwenda kuangalia juu ya maana za kiroho zilizofichika katika mavazi ya Kuhani Mkuu. Haruni alipaswa kuyavaa mavazi haya pamoja na watoto wake. Kwa...
Ndani ya Hema Takatifu la Kukutania kulikuwa kumegawanyika katika sehemu kuu mbili: Mahali Patakatifu na Patakatifu pa Patakatifu. Kulikuwa na pazia kati ya sehemu...